Pregnancy Aug 12, 2024

Kwa Nini Mama Mjamzito Hapaswi Kulala Chali?

Medikea Doctor

Medikea Doctor

Medical Expert

5854
Kwa Nini Mama Mjamzito Hapaswi Kulala Chali?

Mabadiliko mbalimbali wakati wa ujauzito hutokea katika afya ya mwanamke. Mabadiliko hayo husabishwa na uwepo wa mtoto kwenye mfuko wa uzazi pamoja na kuongeza kwa homoni

Mfuko wa uzazi huwa usawa wa kitovu ujauzito unapofikia wiki 20 na kuendelea. Uzito wa mtoto pamoja na ukubwa wa mfuko wa uzazi husababisha mgandamizo mkubwa kwenye mishipa mikubwa ya damu. Mishipa hii hutoa damu kwenye moyo na kusambaza sehemu za chini za mwili na mshipa mwingine hutoa damu sehemu za chini za mwili na kuirudisha kwenye moyo.

Mama mjamzito anapolala chali mfuko wa uzazi hukandamiza hiyo mishipa ya damu hivyo kupunguza uwezo wa kusafirisha damu. Kitendo ambacho husababisha shinikizo la damu (presha) kushuka. Hali hiyo husababisha mama kusikia kizunguzungu, kichefuchefu na hata kupoteza fahamu. Hali hiyo inaweza kuleta madhara makubwa kwa mama na mtoto aliyeko tumboni iwapo hatua za haraka hazitachukuliwa .

Ili kuepuka madhara yatokanayo na hali hiyo mama yeyote mjamzito anashauriwa kulala upande wa kushoto ujauzito unapofika majuma 20. Kwa maswali zaidi kuhusu kizunguzungu and kichefuchefu cha mara kwa mara wakati wa ujauzito wasiliana na Daktari wa uzazi kupitia Medikea App.

Related Articles

Dalili za Mimba Wiki ya Kwanza
Pregnancy

Dalili za Mimba Wiki ya Kwanza

Ujauzito ni mchakato wa kibaiologia ambao unahusisha mabadiliko makubwa katika mwili wa mwanamke. Katika wiki ya kwanza, ...

21227
Feb 25, 2025
Read More
Jinsi ya Kupunguza Kichefuchefu na Kutapika wakati wa Ujauzito
Pregnancy

Jinsi ya Kupunguza Kichefuchefu na Kutapika wakati wa Ujauzito

Jifunze njia za kupunguza Kichefuchefu na Kutapika wakati wa Ujauzito⁣

10891
Aug 28, 2024
Read More
Je ni sawa kuendelea kunyonyesha mtoto wakati una mimba nyingine?
Pregnancy

Je ni sawa kuendelea kunyonyesha mtoto wakati una mimba nyingine?

Makala hii inaelezea kwa kina zaidi⁣

9364
Aug 28, 2024
Read More

More Health Insights

Manjano Kwa Watoto Wachanga: Sababu, Dalili za Hatari na Matibabu.
Watoto

Manjano Kwa Watoto Wachanga: Sababu, Dalili za Hatari na Matibabu.

Homa ya Manjano ni nini na inasababishwa na nini?

11592
May 20, 2023
Read More
Mpox: Dalili, Kinga, na Hatua za Kuchukua
Viral diseases

Mpox: Dalili, Kinga, na Hatua za Kuchukua

Mpox ni ugonjwa wa virusi uliokuwa gumzo hivi karibuni nchini Tanzania. Je, unazijua dalili na njia za kujikinga? Soma z ...

1183
Mar 12, 2025
Read More
Saratani ya kizazi
Women

Saratani ya kizazi

Saratani ya kizazi, dalili na tiba.

283
Sep 6, 2023
Read More