Chronic diseases Aug 2, 2024

Figo kufeli kwa mgonjwa wa kisukari

Medikea Clinic

Medikea Clinic

Medical Expert

588
Figo kufeli kwa mgonjwa wa kisukari

Tangulizi

Kisukari ni hali ya mwili kushindwa kutoa insulini ya kutosha (homoni inayosaidia kudhibiti viwango vya sukari kwenye damu). Sukari ya damu inapokuwa juu huweza kuharibu mishipa ya damu, hivyo mishipa ya damu kushindwa kufanya kazi na kusababisha shinikizo la damu ambalo linaweza kuharibu figo.

Kazi kuu ya figo ni kuchuja taka na maji ya ziada kutoka kwenye damu ili kutengeneza mkojo. Pia husaidia kudhibiti shinikizo la damu na kutengeneza homoni ambazo mwili unahitaji ili kuwa na afya njema. Ugonjwa wa kisukari ndio sababu kuu ya ugonjwa wa figo. Takribani mtu mzima mmoja kati ya watatu wenye ugonjwa wa figo huwa na ugonjwa wa kisukari.

Ugonjwa wa kisukari unaweza kusababisha kufeli kwa figo, ambayo ndiyo hatua ya mwisho ya ugonjwa wa figo. Kushindwa au kufeli kwa figo ni hali inayotishia maisha kwa mgonjwa.

SABABU ZINAZOPELEKEA KUFELI KWA FIGO KWA MGONJWA WA KISUKARI:

  1. Sukari ya juu ya damu isiyodhibitiwa (hyperglycemia).
  2. Shinikizo la damu lisilodhibitiwa (hypertension).
  3. Historia ya familia ya ugonjwa wa kisukari na ugonjwa wa figo.
  4. Uvutaji wa sigara.
  5. Cholesterol ya juu ya damu.
  6. Unene kupita kiasi.

DALILI ZA KUFELI KWA FIGO KWA MGONJWA WA KISUKARI:

Katika hatua za mwanzo za ugonjwa wa figo uliosababishwa na kisukari mara nyingi dalili huwa hazionekani, lakini katika hatua za baadae mgonjwa anaweza kuwa na dalili kama vile:

  • Shinikizo la juu la damu.
  • Kuvimba kwa miguu, vifundoni, mikono au macho.
  • Mkojo wenye povu
  • Kuchanganyikiwa au ugumu wa kufikiri
  • Upungufu wa pumzi
  • Kupoteza hamu ya kula
  • Uchovu na udhaifu
  • Kichefuchefu na kutapika

MATIBABU YA KUFELI KWA FIGO KWA MGONJWA WA KISUKARI:

Kufeli au kushindwa kwa figo ni hatua ya mwisho ya ugonjwa wa figo na matibabu huwa ni pamoja na:

  • Dialysis ya figo: Tiba hii huondoa taka na maji ya ziada kutoka kwenye damu. Hemodialysis huchuja damu nje ya mwili kwa kutumia mashine ambayo inafanya kazi ya figo. Kwa hemodialysis, unaweza kutembelea kituo cha dialysis takribani mara tatu kwa wiki. Au unaweza kufanyiwa dialysis nyumbani na mwangalizi aliyefunzwa. Na kila kipindi huchukua takribani masaa matatu hadi matano.

  • Upandikizaji wa figo: wakati mwingine figo inapofeli au kushindwa, matibabu bora huwa ni upandikizaji wa figo au upandikizaji wa figo-kongosho. Ambapo mgonjwa hufanyiwa uchunguzi ili kujua kama anaweza kufanyiwa upasuaji.

  • Matibabu au usimamizi wa dalili: Kwa mgonjwa ambaye hataki kufanyiwa dialysis au kupandikiza figo, huweza kufanyiwa matibabu ya zile dalili anazoziona ili kumuweka vizuri kwa miezi michache atakayoishi.

VITU VYA KUFANYA KUPUNGUZA HATARI YA KUFELI KWA FIGO KWA MGONJWA WA KISUKARI:

  • Kukutana na timu yake ya afya mara kwa mara,

  • Kupata matibabu ya ugonjwa wa kisukari

  • Kudhibiti shinikizo la damu

  • Kuwa na uzito wa wastani kiafya

  • Kuacha kuvuta sigara

Related Articles

Kupungua Kwa Kumbukumbu: Sababu Na Jinsi Ya Kukabiliana Nayo
Chronic diseases

Kupungua Kwa Kumbukumbu: Sababu Na Jinsi Ya Kukabiliana Nayo

Una wasiwasi kuhusu kupungua kwa kumbukumbu kwako au kwa mpendwa? Pata ushauri wa kitaalam kupitia application ya afya y ...

522
Feb 25, 2025
Read More
Dalili za awali za kisukari: Jinsi ya Kutambua na Kuchukua Hatua
Chronic diseases

Dalili za awali za kisukari: Jinsi ya Kutambua na Kuchukua Hatua

Utafiti wa hivi karibuni umeonyesha kuwa watu wengi hukosa fursa ya kugundua ugonjwa huu mapema kwa sababu ya kutojua da ...

152
Feb 25, 2025
Read More
Jifunze Siri ya Ngozi Yenye Afya.
Chronic diseases

Jifunze Siri ya Ngozi Yenye Afya.

Ijue siri ya ngozi yenye afya.⁣

270
Jan 29, 2025
Read More

More Health Insights

Je ni sawa kuendelea kunyonyesha mtoto wakati una mimba nyingine?
Pregnancy

Je ni sawa kuendelea kunyonyesha mtoto wakati una mimba nyingine?

Makala hii inaelezea kwa kina zaidi⁣

4423
Aug 28, 2024
Read More
Ugonjwa wa Pumu: Vihatarishi, Dalili na Matibabu
Watoto

Ugonjwa wa Pumu: Vihatarishi, Dalili na Matibabu

Je wajua? Katika Tanzania, pumu ni tatizo kubwa la afya ya umma. Utafiti unaonyesha kuwa asilimia 10% hadi 20% ya watoto ...

1051
Feb 26, 2024
Read More
Pumu Ya Ngozi Kwa Watoto: Visababishi, Dalili Na Matibabu
Watoto

Pumu Ya Ngozi Kwa Watoto: Visababishi, Dalili Na Matibabu

Pumu ya ngozi ni ugonjwa wa ngozi unaofanya ngozi kuwasha, kuvimba na kuweka viupele vidogovidogo vyenye rangi nyekundu ...

4748
May 15, 2024
Read More