MPOX: DALILI, KINGA, NA HATUA ZA KUCHUKUA
Mpox ni ugonjwa unaosababishwa na virusi na huambukizwa kupitia kugusana moja kwa moja na mtu aliyeambukizwa au kwa njia ya wanyama. Ugonjwa huu unaweza kuathiri mtu yeyote, na ni muhimu kuchukua tahadhari ili kuzuia maambukizi.
DALILI ZA MPOX
Dalili za Mpox hujitokeza kati ya siku 3 hadi 17 baada ya kuambukizwa. Dalili hizo ni pamoja na:
- Upele wenye usaa unaoweza kupatikana mikononi, miguu, kifuani, usoni, mdomoni au karibu na sehemu za siri, ikiwemo uume, korodani, na ukeni.
- Homa
- Baridi
- Kuvimba Tezi
- Uchovu
- Maumivu ya misuli na mgongo
- Maumivu ya Kichwa
- Dalili za mfumo wa hewa (kwa mfano, maumivu ya koo, kuziba kwa pua, au kikohozi)
JINSI YA KUJIKINGA NA MPOX
Ili kujikinga na ugonjwa wa Mpox, ni muhimu kufuata hatua zifuatazo:
- Epuka kugusana moja kwa moja na mtu mwenye dalili za Mpox.
- Usitumie vitu vya mtu aliyeambukizwa, kama vile nguo, matandiko, au vyombo vya kula.
- Osha mikono mara kwa mara kwa maji tiririka na sabuni au tumia vitakasa mikono.
- Wahudumu wa afya wanapaswa kutumia vifaa vya kujikinga wanapowahudumia wagonjwa.
NINI CHA KUFANYA KAMA UNA DALILI ZA MPOX?
Ikiwa una dalili za Mpox, unashauriwa:
- Kutembelea kituo cha huduma za afya kwa uchunguzi na matibabu.
- Kupiga simu kwa namba 199 bila malipo kwa msaada wa kitaalamu.
- Kuepuka kuwasiliana kwa karibu na watu wengine ili kuzuia maambukizi zaidi.
HITIMISHO
Mpox ni ugonjwa unaoweza kudhibitiwa ikiwa tahadhari zitachukuliwa kwa umakini. Medikea inakupa fursa ya kupata ushauri wa kitabibu moja kwa moja kupitia jukwaa letu la afya mtandaoni na app ambayo inapatikana playstore na appstore. Jiunge nasi kwa huduma za haraka na bora ili kuhakikisha unapata msaada unaohitaji kwa wakati muafaka.
Tembelea Medikea leo kwa huduma bora za afya.