Wellness Aug 12, 2024

Unapokwenda kumuona daktari huwa unajielezaje?

Medikea Doctor

Medikea Doctor

Medical Expert

46
Unapokwenda kumuona daktari huwa unajielezaje?

Inawezekana umekwenda mara kadhaa kuonana na daktari kutokana na maradhi yanakusumbua. Lakini je umekuwa ukijieleza kwa sasa au umekuwa ukipata wakati mgumu kutoa maelezo yako kwa daktari.

Katika afya tunaamini kuwa hakuna kipimo chochote ambacho kimeweza kuchukua nafasi ya maelezo ya mgonjwa. Kwa maana nyingine ni kuwa maelezo yako kwa daktari ni muhimu sana katika kubaini ugonjwa wako.

Kwa kiasi kikubwa daktari anaweza kubaini ugonjwa wako kutokana na maelezo yako. Ni muhimu kutoa maelezo kwa ufasaha.

Ujieleze vipi?

Kumbuka unapokwenda kwa daktari una kuwa maradhi na sio ugonjwa. Ni wajibu wako kumueleza daktari maradhi yanakusumbua. Kutokana na maradhi yako ndipo daktari anaweza kujua unaumwa ugonjwa gani.

Maradhi ni tofauti na ugonjwa. Maumivu ya kichwa, homa, kichefuchefu, kutapika, kuharisha hayo ni maradhi. Wakati malaria, pneumonia, Kisukari hayo ni magonjwa.

Hivyo ukifika kwa daktari mweleze maradhi yako na sio ugonjwa.

Mfano mazungumzo ya mwazo baada ya salaam na utambulisho daktari anaweza kukuuliza

"Nini kimefanya uje hospitali leo au nini kimefanya uje kuniona"

Jibu lako linaweza kuwa: Ninasumbuliwa sana na maumivu ya kichwa leo siku ya tatu sasa. Unaweza kuongezea iwapo una dalili nyingine.

Epuka kutoa maelezo kama nimekuja kupima malaria au typhoid au presha. Maelezo kama hayo hayana msaada. Wasiliana na daktari kuirahisi kupitia App ya Medikea iliyopo Android na iOS.

Baada ya kuelezea maradhi yako makuu,maelezo mengine jibu kwa kadri daktari anavyokuuliza maswali.

Related Articles

Jinsi ya Kupunguza Stress
Wellness

Jinsi ya Kupunguza Stress

Una dalili za stress na unahitaji ushauri wa kitaalam? Wasiliana na madaktari wetu kupitia programu ya Medikea. Tutakusa ...

77
Feb 25, 2025
Read More
Wegovy (Ozempic): Dawa mpya za kupunguza uzito, inafanya kazi? Je ni salama?
Wellness

Wegovy (Ozempic): Dawa mpya za kupunguza uzito, inafanya kazi? Je ni salama?

Ozempic, wegovy, maunjaro na dawa nyingine za kupunguza uzito

636
Aug 9, 2024
Read More

More Health Insights

Nafasi Ya Usingizi Katika Kupunguza Uzito Na Namna Ya Kuiboresha
Afya na Usalama

Nafasi Ya Usingizi Katika Kupunguza Uzito Na Namna Ya Kuiboresha

Makala hii inaelezea umuhimu wa usingizi katika kupunguza uzito. Inafafanua jinsi usingizi unavyoathiri homoni za njaa, ...

0
Mar 28, 2025
Read More
Jinsi Ya Kuvunja Mwamba Wa Kupunguza Uzito Weight Loss Plateau
Afya na Usalama

Jinsi Ya Kuvunja Mwamba Wa Kupunguza Uzito Weight Loss Plateau

Blogu hii inahusu njia za kuvunja mwamba wa kupunguza uzito (weight loss plateau). Inatoa mbinu mbalimbali kama vile kur ...

0
Mar 28, 2025
Read More
Kwa Nini Mama Mjamzito Hapaswi Kulala Chali?
Pregnancy

Kwa Nini Mama Mjamzito Hapaswi Kulala Chali?

Ujauzito unakuja na changamoto tofauti kutokana na mabadiliko ya mwili yanayotokea. Soma makala hii kujifunza!

1636
Aug 12, 2024
Read More