Wellness Aug 12, 2024

Unapokwenda kumuona daktari huwa unajielezaje?

Medikea Doctor

Medikea Doctor

Medical Expert

125
Unapokwenda kumuona daktari huwa unajielezaje?

Inawezekana umekwenda mara kadhaa kuonana na daktari kutokana na maradhi yanakusumbua. Lakini je umekuwa ukijieleza kwa sasa au umekuwa ukipata wakati mgumu kutoa maelezo yako kwa daktari.

Katika afya tunaamini kuwa hakuna kipimo chochote ambacho kimeweza kuchukua nafasi ya maelezo ya mgonjwa. Kwa maana nyingine ni kuwa maelezo yako kwa daktari ni muhimu sana katika kubaini ugonjwa wako.

Kwa kiasi kikubwa daktari anaweza kubaini ugonjwa wako kutokana na maelezo yako. Ni muhimu kutoa maelezo kwa ufasaha.

Ujieleze vipi?

Kumbuka unapokwenda kwa daktari una kuwa maradhi na sio ugonjwa. Ni wajibu wako kumueleza daktari maradhi yanakusumbua. Kutokana na maradhi yako ndipo daktari anaweza kujua unaumwa ugonjwa gani.

Maradhi ni tofauti na ugonjwa. Maumivu ya kichwa, homa, kichefuchefu, kutapika, kuharisha hayo ni maradhi. Wakati malaria, pneumonia, Kisukari hayo ni magonjwa.

Hivyo ukifika kwa daktari mweleze maradhi yako na sio ugonjwa.

Mfano mazungumzo ya mwazo baada ya salaam na utambulisho daktari anaweza kukuuliza

"Nini kimefanya uje hospitali leo au nini kimefanya uje kuniona"

Jibu lako linaweza kuwa: Ninasumbuliwa sana na maumivu ya kichwa leo siku ya tatu sasa. Unaweza kuongezea iwapo una dalili nyingine.

Epuka kutoa maelezo kama nimekuja kupima malaria au typhoid au presha. Maelezo kama hayo hayana msaada. Wasiliana na daktari kuirahisi kupitia App ya Medikea iliyopo Android na iOS.

Baada ya kuelezea maradhi yako makuu,maelezo mengine jibu kwa kadri daktari anavyokuuliza maswali.

Related Articles

Jinsi ya Kupunguza Stress
Wellness

Jinsi ya Kupunguza Stress

Una dalili za stress na unahitaji ushauri wa kitaalam? Wasiliana na madaktari wetu kupitia programu ya Medikea. Tutakusa ...

338
Feb 25, 2025
Read More
Wegovy (Ozempic): Dawa mpya za kupunguza uzito, inafanya kazi? Je ni salama?
Wellness

Wegovy (Ozempic): Dawa mpya za kupunguza uzito, inafanya kazi? Je ni salama?

Ozempic, wegovy, maunjaro na dawa nyingine za kupunguza uzito

1305
Aug 9, 2024
Read More

More Health Insights

Pumu Ya Ngozi Kwa Watoto: Visababishi, Dalili Na Matibabu
Watoto

Pumu Ya Ngozi Kwa Watoto: Visababishi, Dalili Na Matibabu

Pumu ya ngozi ni ugonjwa wa ngozi unaofanya ngozi kuwasha, kuvimba na kuweka viupele vidogovidogo vyenye rangi nyekundu ...

5908
May 15, 2024
Read More
Unapokwenda kumuona daktari huwa unajielezaje?
Wellness

Unapokwenda kumuona daktari huwa unajielezaje?

Maongezi mazuri baina ya mgonjwa na daktari ni muhimu sana kuhakikisha tiba stahiki. Soma makala hii kuelewa njia nzuri ...

125
Aug 12, 2024
Read More
“Tayari Nina Watoto Lakini Sipati Tena Mimba” - Ugumba wa aina ya pili
Women

“Tayari Nina Watoto Lakini Sipati Tena Mimba” - Ugumba wa aina ya pili

Fahamu sababu zinazosababisha ugumba kwa wenza ambao wameshapata Mtoto awali

673
May 15, 2024
Read More