Women Aug 12, 2024

Huu Ndio Utaratibu wa Kufanya Mazoezi Baada Ya Kujifungua Kwa Upasuaji

Medikea Doctor

Medikea Doctor

Medical Expert

2355
Huu Ndio Utaratibu wa Kufanya Mazoezi Baada Ya Kujifungua Kwa Upasuaji

Kuwahi kutembea na kurudia shughuli za kawaida na za kabla ya ujauzito na kujifungua pamoja na mazoezi mara tu daktari anapoona ni salama inasaidia kuimarisha afya ya mama na kupunguza magonjwa yatokanayo na kukaa muda mrefu.

Hata hivyo wanawake wenye matatizo yafuatayo wanashauriwa kuchelewa kidogo kurudia mazoezi na shughuli za awali kabla ya ujauzito na wapate idhini ya daktari kabla ya kuanza kutembea au kufanya mazoezi

• Wenye magonjwa mengine (upungufu wa damu, magonjwa ya moyo na njia ya hewa, matatizo ya damu kuganda kwenye mishipa) • Wana maumivu na bado wanahitaji dawa za kutuliza maumivu • Madhara wakati wa na baada ya upasuaji (kichefuchefu na kutapika, kidonda kutopona vizuri, ganzi, mkojo kutoka wenyewe)

Sasa kwa wale ambao hawana matatizo na wale ambao wamepata idhini kutoka kwa daktari utaratibu wa kufanya mazoezi uko hivi :

▪️Wiki ya 1 hadi wiki ya 2 baada ya kuruhusiwa

  • Tembea angalau dakika 10 kwa siku mara nyingi kadri uwezavyo na unaweza kuongeza muda kadri unavyoweza

  • Panda ngazi nyumbani au hospital ukiwa na msaidizi

  • Usinyanyue kitu kingine chochote chenye uzito zaidi ya uzito wa mtoto

▪️Baada ya wiki 3 na kuendelea

Fanya mazoezi ya kuimarisha nyonga na tumbo

Angalia video za mazoezi yafuatayo YouTube (Pelvic tilting and abdominal curl,Lower back lift, Oblique curls, Lateral tilts, Kegel pelvic floor muscle). Fanya mazoezi katika kila kundi kuanzia mara 10 hadi 12 kwa kuanza taratibu na kuongeza kadri uwezavyo.

▪️Baada ya wiki 6 na kuendelea

-Wanawake ambao hapo awali walikuwa wanafanya mazoezi kwenye gym na vilabu vya mazoezi taratibu na kwa uangalifu wanaweza kurudia mazoezi yao kwa kuanza na settings za chini kwenye mashine za mazoezi

-Baada ya wiki sita wanawake wote wanaweza kufanya mazoezi ya kiwango cha kati (moderate intensity physical activity) kama inavyopendekezwa kwa watu wengine ambayo ni kufanya mazoezi hayo kwa muda wa dakika 150 hadi 300 kwa wiki)

Kwa msaada wa karibu wa mtaalamu wa mazoezi (Physiotherapist) pakua app ya Medikea ku chat au wasiliana na Medikea Clinic kupitia 0763100093 ili kupata mazoezi tiba clinic au nyumbani!

Related Articles

Uti ni nini? Dalili zake na jinsi ya kujikinga
Women

Uti ni nini? Dalili zake na jinsi ya kujikinga

UTI inasababishwa na nini, dalili zake na jinsi ya kujinga

30600
Nov 6, 2024
Read More
Ijue siri kubwa ya kuzalisha maziwa ya kutosha
Women

Ijue siri kubwa ya kuzalisha maziwa ya kutosha

Soma kujua jinsi ya kuzalisha maziwa ya kutosha kwa mama anaenyonyesha!

515
Aug 28, 2024
Read More
“Tayari Nina Watoto Lakini Sipati Tena Mimba” - Ugumba wa aina ya pili
Women

“Tayari Nina Watoto Lakini Sipati Tena Mimba” - Ugumba wa aina ya pili

Fahamu sababu zinazosababisha ugumba kwa wenza ambao wameshapata Mtoto awali

421
May 15, 2024
Read More

More Health Insights

Manjano Kwa Watoto Wachanga: Sababu, Dalili za Hatari na Matibabu.
Watoto

Manjano Kwa Watoto Wachanga: Sababu, Dalili za Hatari na Matibabu.

Homa ya Manjano ni nini na inasababishwa na nini?

6049
May 20, 2023
Read More
Upungufu wa damu wakati wa ujauzito
Women

Upungufu wa damu wakati wa ujauzito

Zifahamu sababu za upungufu wa damu wakati wa ujauzito.

1983
Mar 12, 2024
Read More
Fahamu Sababu Za Kutokwa Na Damu Baada Ya Kufanya Mapenzi Au Kujamiiana
Women

Fahamu Sababu Za Kutokwa Na Damu Baada Ya Kufanya Mapenzi Au Kujamiiana

Kutokwa na damu wakati wa kujamiiana yaweza kuleta wasiwasi ila pia ni kawaida. Zaidi ya asilimia 9% ya wanawake hupata ...

4575
May 4, 2024
Read More