Pregnancy Aug 28, 2024

Je ni sawa kuendelea kunyonyesha mtoto wakati una mimba nyingine?

Medikea Doctor

Medikea Doctor

Medical Expert

2691
Je ni sawa kuendelea kunyonyesha mtoto wakati una mimba nyingine?

Kuna wakati inatokea mama anakugundua kuwa ni mjamzito wakati bado ananyonyesha. Mtoto anayenyonyeshwa anaweza kuwa mdogo hajafikia umri wa kuachishwa au mama mwenyewe anakuwa bado anapenda kumnyonyesha mtoto wake. Ikiwa mimba ni ya kawaida na yenye afya, inachukuliwa kuwa ni salama kabisa kuendelea kunyonyesha katika kipindi chote cha mimba.

Katika kipindi hiki mama hana haja ya kuwa na wasiwasi kwamba maziwa yake yatakuwa hayana virutubisho vya kumtosha mtoto wake anayenyonya. Pia haitaji kuwa na wasiwasi kwamba unyonyeshaji unaweza kuathiri mimba yake.

Kuongezeka kwa uchovu na kichefuchefu wakati wa ujauzito inaweza kuwa changamoto kwa mama kijacho. Hata hivyo mama anashauriwa kupata muda wa kutosha wa kupumzika na kula mlo kamili. Ni muhimu kula mlo kamili ili kuhakikisha unapata virutubisho vya kutosha ili kukufanya uwe na afya njema.

Wakati wa ujauzito kiwango cha maziwa kinaweza kupungua pia radha ya maziwa huwa inabadalika. Mambo haya mawili yanaweza kusababisha mtoto mwenyewe kukataa kunyonya. Hata hivyo kama mtoto bado ni mchanga sana ni vizuri kuendelea kumnyonyesha ili asikose virutubisho muhimu kutoka kwenye maziwa ya mama.

Je wakati gani unashauriwa kumuachisha mtoto kama una mimba nyingine? Unaweza kushauriwa kuachishwa mtoto iwapo:

  • uko katika hatari ya kupata uchungu mapema,

  • mimba iko katika hatari ya kutoka au

  • daktari amekushauri USIFANYE tendo la ndoa wakati wa ujauzito.

  • Unapata maumivu ya tumbo yanayoambatana na kutoka damu

Zingatia:

  1. Ni muhimu kutumia njia za uzazi wa mpango ili kuepuka kupata ujauzito usiotarajiwa ili kuepuka madhara yatokanayo na ujauzito na uzazi. Na unaweza kuongea na daktari kujua njia bora ya uzazi wa mpango bora wakati unanyonyesha kupitia Medikea App.

  2. Ni muhimu kupata lishe Bora ili kuepuka kupata utapia mlo hivyo kujiweka katika hatari ya ujauzito wako kuharibika. Lishe ni MUHIMU, MUHIMU sana wakati huu.

Related Articles

Dalili Za Mimba Wiki Ya Kwanza
Pregnancy

Dalili Za Mimba Wiki Ya Kwanza

Ujauzito ni mchakato wa kibaiologia ambao unahusisha mabadiliko makubwa katika mwili wa mwanamke. Katika wiki ya kwanza, ...

212
Feb 25, 2025
Read More
Jinsi ya Kupunguza Kichefuchefu na Kutapika wakati wa Ujauzito
Pregnancy

Jinsi ya Kupunguza Kichefuchefu na Kutapika wakati wa Ujauzito

Jifunze njia za kupunguza Kichefuchefu na Kutapika wakati wa Ujauzito⁣

3278
Aug 28, 2024
Read More
Kwa Nini Mama Mjamzito Hapaswi Kulala Chali?
Pregnancy

Kwa Nini Mama Mjamzito Hapaswi Kulala Chali?

Ujauzito unakuja na changamoto tofauti kutokana na mabadiliko ya mwili yanayotokea. Soma makala hii kujifunza!

1446
Aug 12, 2024
Read More

More Health Insights

Huu Ndio Utaratibu wa Kufanya Mazoezi Baada Ya Kujifungua Kwa Upasuaji
Women

Huu Ndio Utaratibu wa Kufanya Mazoezi Baada Ya Kujifungua Kwa Upasuaji

Huu Ndio Utaratibu Wa Kufanya Mazoezi Baada Ya Kujifungua Kwa Upasuaji

1624
Aug 12, 2024
Read More
Saratani ya shingo ya kizazi
Women

Saratani ya shingo ya kizazi

Saratani ya shingo ya kizazi inasababishwa na nini, dalili, na matibabu yake.

4904
Aug 29, 2023
Read More
Tiba ya bawasiri (Hemorrhoids)
Men

Tiba ya bawasiri (Hemorrhoids)

Bawasiri inasababishwa na nini, dalili zake, na jinsi ya kuzitibu

6779
Aug 30, 2023
Read More