Pregnancy Aug 28, 2024

Jinsi ya Kupunguza Kichefuchefu na Kutapika wakati wa Ujauzito

Medikea Doctor

Medikea Doctor

Medical Expert

3278
Jinsi ya Kupunguza Kichefuchefu na Kutapika wakati wa Ujauzito

Wanawake wengine hawapati matatizo yoyote wakati wa ujauzito, wakati wengine hukubaliwa na maradhi wakati wote wa ujauzito. Hata hivyo habari njema ni kwamba chochote kinachokusumbua, kuna njia za kukabiliana nayo. ⁣

Mojawapo ya maradhi yanayosumbua wajawazito wengi ni kichefuchefu na kutapika wakati wa ujauzito. Bahati nzuri kuwa tatizo hili halisababishi madhara yoyote kwa mama wala kwa mtoto aliyeko tumboni.⁣

Kichefuchefu hujitokeza kuanzia wiki nne hadi nane za mwanzo wa ujauzito. Kinaweza kuendelea hadi wiki 13 mpaka 14 za ujauzito. Wakati mwingine kichefuchefu kinaweza kuanza mapema zaidi na kuendelea kwa muda mrefu bila kukoma. ⁣

Nini husababisha kichefuchefu na kutapika wakati wa ujauzito? Mpaka sasa hakuna sababu ya moja kwa moja inayojulikana kusababisha kichefuchefu na kutapika wakati wa ujauzito. Hata hivyo ina hisiwa kuwa mabadiliko ya homoni yanatokea wakati wa ujauzito huenda yanasababisha hali hiyo.⁣

Njia 7 za kupunguza kichefuchefu na kutapika wakati wa ujauzito.

  • Kunywa maji mengi hasa baada ya milo. Usinywe maji mengi wakati wa kula.⁣

  • Kula kidogo kidogo na mara kwa mara, epuka kula chakula kingi wakati mmoja.⁣

  • Kula chakula kidogo wakati wa asubuhi kabla ya kuamka kitandani.⁣

  • Epuka vyakula vyenye mafuta mafuta na vyakula vilivyokaangwa.⁣

  • Tafuna au kunywa chai yenye tangawizi.⁣

  • Lala na pata muda wa kutosha wa kupumzika ⁣

  • Kula vyakula vilivyokaushwa mfano cookies.⁣

Iwapo hutopata nafuu baada ya kufanya hayo yote chati na daktari kupitia App ya Medikea na atakuandikia dawa ambayo inaweza kuzuia kichefuchefu na kutapika wakati wa ujauzito.

Related Articles

Dalili Za Mimba Wiki Ya Kwanza
Pregnancy

Dalili Za Mimba Wiki Ya Kwanza

Ujauzito ni mchakato wa kibaiologia ambao unahusisha mabadiliko makubwa katika mwili wa mwanamke. Katika wiki ya kwanza, ...

212
Feb 25, 2025
Read More
Je ni sawa kuendelea kunyonyesha mtoto wakati una mimba nyingine?
Pregnancy

Je ni sawa kuendelea kunyonyesha mtoto wakati una mimba nyingine?

Makala hii inaelezea kwa kina zaidi⁣

2691
Aug 28, 2024
Read More
Kwa Nini Mama Mjamzito Hapaswi Kulala Chali?
Pregnancy

Kwa Nini Mama Mjamzito Hapaswi Kulala Chali?

Ujauzito unakuja na changamoto tofauti kutokana na mabadiliko ya mwili yanayotokea. Soma makala hii kujifunza!

1446
Aug 12, 2024
Read More

More Health Insights

JE, NI KWELI UNAHITAJI KUNYWA VIDONGE VYA VITAMINI NA “SUPPLEMENTS” KILA SIKU?
Women

JE, NI KWELI UNAHITAJI KUNYWA VIDONGE VYA VITAMINI NA “SUPPLEMENTS” KILA SIKU?

Fahamu ni wakati gani unatakiwa utumie virutubisho hivi

569
Feb 20, 2024
Read More
Je, ni sawa kufanya ngono wakati wa ujauzito?
Pregnancy

Je, ni sawa kufanya ngono wakati wa ujauzito?

Baada ya watu wengi kuuliza swali hili, ufafunuzi huu utasaidia watu wengi wawezi kufahamu.

1054
Aug 12, 2024
Read More
Fahamu dalili na tiba za ugonjwa wa kisukari
Men

Fahamu dalili na tiba za ugonjwa wa kisukari

Ufahamu ugonjwa wa kisukari

10220
Nov 6, 2023
Read More