Women Nov 6, 2024

Uti ni nini? Dalili zake na jinsi ya kujikinga

Dr Saida Ally

Dr Saida Ally

Medical Expert

25634
Uti ni nini? Dalili zake na jinsi ya kujikinga

Tangulizi

UTI (Urinary tract infection) ni ugonjwa wa maambukizi katika mfumo wa mkojo na maambukizi haya yanasababishwa na viumbe kama bakteria, fangasi na virus. Mara nyingi bakteria wanaoingia kwenye mfumo wa mkojo hutolewa na mwili. Wakati mwingine bakteria wanaweza zidi kinga ya mwili na kusababisha maambukizi hayo. UTIs inaweza athiri mrija wa mkojo (urethra), kibofu cha mkojo na figo.

Una dalili za UTI? Usipoteze muda - wasiliana na daktari bingwa kupitia application ya Medikea kwenye iOS au android sasa. Tumia simu yako kupata ushauri wa haraka na wa kitaalamu bila foleni wala usumbufu.

MFUMO WA MKOJO

Mfumo wa mkojo ni mfumo wa mwili unaotumika kuondoa uchafu na maji ya ziada. Mfumo huu una majukumu muhimu:

  • Kusafisha damu na kuondoa sumu
  • Kudhibiti usawa wa madini mwilini
  • Kutengeneza homoni muhimu
  • Kusaidia kudhibiti shinikizo la damu

Mfumo huu unaundwa na:

  1. Figo (zinasafisha damu)
  2. Ureta (inasafirisha mkojo)
  3. Kibofu cha mkojo (kuhifadhi)
  4. Urethra (kutoa mkojo nje)

UTI INASABABISHWA NA NINI?

Mara nyingi UTI zinasababishwa na bakteria aitwaye Escherichia coli (E. coli) ambayo husababisha 80% ya kesi zote. Vyanzo vingine ni:

Bakteria Klebsiella pneumoniae Staphylococcus saprophyticus Chlamydia na Mycoplasma (hususan kwa maambukizi ya mfumo wa uzazi)

Muhimu: UTI inayosababishwa na Chlamydia na Mycoplasma inahitaji wenza wote kupata tiba pamoja.

Takwimu za Kimataifa zinaonyesha zaidi ya watu milioni 8.1 wanaathiriwa na ugonjwa huu kila mwaka.

DALILI ZA UTI

  • Kukojoa mara kwa mara na maumivu wakati wa kukojoa
  • Kuhisi kuunguzwa/kuwashwa na mkojo kwenye kibofu au mrija wa mkojo
  • Maumivu ya misuli na tumbo
  • Mkojo kuwa na harufu mbaya na kubadilika rangi (nyeusi au rangi ya mawingu)
  • Maumivu mgongoni au kwenye mbavu (kwa maambukizi ya figo)
  • Kichefuchefu na kutapika
  • Kushikwa na hamu ya kukojoa ila mkojo unatoka kidogo

Dalili za Hatari Zaidi:

  • Homa ya juu
  • Kutetemeka
  • Mkojo wenye damu
  • Maumivu makali ya mgongo
  • Kutapika kwa kiwango kikubwa

NI WATU GANI WALIO KATIKA HATARI YA KUPATA UTI?

  • Watu wenye kutumia mpira wa mkojo kwa muda mrefu na pempas

  • Watu wenye matatizo ya mfumo wa mkojo (figo, mirija, kibofu)

  • Watumiaji wa njia fulani za uzazi (diaphragm, spermicides, kondomu)

  • Watu wenye mahusiano ya kimapenzi yanayoweza kuhamisha bakteria

  • Wanawake (kutokana na maumbile yao)

  • Wajawazito

  • Watu wenye kisukari

  • Watu wenye mfumo dhaifu wa kinga

KWANINI WANAWAKE NDO WAHANGA WAKUBWA?

  1. Urethra ya wanawake ni fupi zaidi (takribani sentimita 4 tu), hivyo bakteria wana safari fupi kufika kibofu
  2. Mrija wa mkojo uko karibu na uke na tupu ya nyuma, maeneo yenye bakteria wengi
  3. Mabadiliko ya homoni wakati wa ujauzito na hedhi Matumizi ya baadhi ya njia za uzazi wa mpango

Kwa wanaume ni nadra kupata UTI, lakini wakipatwa, dalili zinaweza kuwa kali zaidi na matibabu magumu zaidi.

KWANINI UNAPATA UTI MARA KWA MARA (UTI SUGU)

  • Mfumo wa kinga dhaifu: Kushindwa kupambana na bakteria
  • Kuwa mwanamke: Hatari kubwa kutokana na maumbile
  • Kukaa na mkojo kwa muda mrefu
  • Mahusiano ya kimapenzi: Kuhamisha bakteria
  • Kutokunywa maji ya kutosha
  • Matumizi yasiyo sahihi ya antibiotiki
  • Mabadiliko ya homoni
  • Masuala ya kiafya kama kisukari

JINSI YA KUJIKINGA NA UTI

  1. Kunywa maji mengi (angalau lita 2-3 kwa siku)
  2. Kukojoa mara kwa mara bila kuchelewa
  3. Kujisafisha vizuri (kutoka mbele kwenda nyuma)
  4. Kuvaa nguo za ndani za pamba na zisizobana
  5. Kukojoa baada ya kujamiiana
  6. Kula vyakula vyenye probiotics
  7. Kudumisha usafi wa maeneo ya siri

ATHARI ZA KUTOKUTIBU UTI KIKAMILIFU

  • Uharibifu wa kudumu wa figo
  • Kuhitaji dialysis
  • Uzazi wa watoto wenye uzito mdogo au kuzaa kabla ya wakati
  • Prostatitis kwa wanaume
  • Sepsis (sumu katika damu)
  • Matatizo ya moyo
  • Shinikizo la damu la juu

PATA MSAADA SASA: Dalili za UTI hazitakiwi kupuuzwa. Kupitia programu ya Medikea kwenye iOS au android, utapata:

  1. Ushauri wa madaktari bingwa ndani ya dakika chache
  2. Mpango wa matibabu unaofaa hali yako
  3. Ufuatiliaji wa karibu wakati wa tiba
  4. Ushauri wa kuzuia UTI kurudi

Pakua programu ya Medikea leo na uanze safari yako ya kupona.

TIBA NA MATIBABU

Tiba ya Haraka:

  1. Antibiotiki zinazofaa
  2. Maji mengi
  3. Dawa za kupunguza maumivu

Tiba ya Muda Mrefu:

  1. Antibiotiki za kuzuia maambukizi
  2. Mabadiliko ya mtindo wa maisha
  3. Ufuatiliaji wa karibu na daktari

Matibabu ya Asili:

  1. Juisi ya cranberry

  2. Probiotics (soma makala kuhusu probiotics hapa)

  3. Maji ya mgogoro

    Kumbuka: Tiba za asili zinapaswa kutumiwa pamoja na ushauri wa daktari

Kumbuka: UTI inaweza kuwa tofauti kwa kila mtu. Ni muhimu kupata uchunguzi wa kitaalamu ili kupata matibabu sahihi yanayofaa hali yako mahususi.

Related Articles

Ijue siri kubwa ya kuzalisha maziwa ya kutosha
Women

Ijue siri kubwa ya kuzalisha maziwa ya kutosha

Soma kujua jinsi ya kuzalisha maziwa ya kutosha kwa mama anaenyonyesha!

249
Aug 28, 2024
Read More
Huu Ndio Utaratibu wa Kufanya Mazoezi Baada Ya Kujifungua Kwa Upasuaji
Women

Huu Ndio Utaratibu wa Kufanya Mazoezi Baada Ya Kujifungua Kwa Upasuaji

Huu Ndio Utaratibu Wa Kufanya Mazoezi Baada Ya Kujifungua Kwa Upasuaji

1865
Aug 12, 2024
Read More
“Tayari Nina Watoto Lakini Sipati Tena Mimba” - Ugumba wa aina ya pili
Women

“Tayari Nina Watoto Lakini Sipati Tena Mimba” - Ugumba wa aina ya pili

Fahamu sababu zinazosababisha ugumba kwa wenza ambao wameshapata Mtoto awali

299
May 15, 2024
Read More

More Health Insights

Vyakula 10 Vyenye Virutubisho Vingi Kwa Kupunguza Uzito (1)
Default
Kwa Nini Mama Mjamzito Hapaswi Kulala Chali?
Pregnancy

Kwa Nini Mama Mjamzito Hapaswi Kulala Chali?

Ujauzito unakuja na changamoto tofauti kutokana na mabadiliko ya mwili yanayotokea. Soma makala hii kujifunza!

1636
Aug 12, 2024
Read More
Imani Potofu Zinazohusiana Na Kupunguza Uzito Ukweli Na Uongo
Afya na Lishe

Imani Potofu Zinazohusiana Na Kupunguza Uzito Ukweli Na Uongo

Maudhui haya yanaondoa imani potofu kuhusu kupunguza uzito, yakieleza ukweli na kutoa suluhisho za kisayansi. Inasisitiz ...

0
Mar 28, 2025
Read More