Women Aug 28, 2024

Ijue siri kubwa ya kuzalisha maziwa ya kutosha

Medikea Doctor

Medikea Doctor

Medical Expert

1396
Ijue siri kubwa ya kuzalisha maziwa ya kutosha

Uzalishaji wa maziwa unategemea kiwango cha homoni ya prolactin kinachopelekwa kwenye maziwa ya mama. Homoni ya prolactin inazalishwa kwa wingi kadri ziwa la mama linavyonyonywa mara nyingi au kukamuliwa mara nyingi. ⁣

⁣ Kwa hiyo siri kubwa kwa mama kupata maziwa ya kutosha ni kuhakikisha mtoto ana nyonya maziwa yake mara nyingi iwezekanavyo hasa siku za mwanzo baada ya mtoto kuzaliwa

Kama inawezekana hakikisha mtoto anaanza kunyonya ndani ya saa moja baada ya kuzaliwa. Katika wiki tatu za mwanzo mtoto anapaswa kunyonya angalau mara 12 kwa siku. ⁣

Kuwahi kumuanzishia mtoto maziwa ya kopo kutaathiri uwezo wako wa kuzalisha maziwa, kwa sababu mtoto atashiba na hivyo kushindwa kunyonya. Kama mwanao anashindwa kunyonya kutokana na ugonjwa au sababu nyingine hakikisha mwenyewe unakamua maziwa yako.⁣

Endapo umemnyonyesha mwanao mara nyingi zaidi na unahisi hupati bado maziwa ya kutosha na mwanao hashibi unaweza kujaribu kutumia baadhi ya vyakula vinavyoongeza maziwa au ongea na daktari wako akuandikie dawa ya kuongeza maziwa. ⁣

Lakini zingatia: Jambo moja muhimu ni kuhakikisha mtoto ananyonya, mvutishe ziwa mara nyingi kadri uwezavyo, angalau mara 12 kwa siku katika kipindi cha wiki tatu za mwanzo. ⁣Kama utafanya hivi na bado unadhani maziwa hayatoshi, tafadhali wasiliana na mtaalamu wetu wa lishe kupitia Medikea App.

Related Articles

Uti ni nini? Dalili zake na jinsi ya kujikinga
Women

Uti ni nini? Dalili zake na jinsi ya kujikinga

UTI inasababishwa na nini, dalili zake na jinsi ya kujinga

40384
Nov 6, 2024
Read More
Huu Ndio Utaratibu wa Kufanya Mazoezi Baada Ya Kujifungua Kwa Upasuaji
Women

Huu Ndio Utaratibu wa Kufanya Mazoezi Baada Ya Kujifungua Kwa Upasuaji

Huu Ndio Utaratibu Wa Kufanya Mazoezi Baada Ya Kujifungua Kwa Upasuaji

3597
Aug 12, 2024
Read More
“Tayari Nina Watoto Lakini Sipati Tena Mimba” - Ugumba wa aina ya pili
Women

“Tayari Nina Watoto Lakini Sipati Tena Mimba” - Ugumba wa aina ya pili

Fahamu sababu zinazosababisha ugumba kwa wenza ambao wameshapata Mtoto awali

673
May 15, 2024
Read More

More Health Insights

Pumu Ya Ngozi Kwa Watoto: Visababishi, Dalili Na Matibabu
Watoto

Pumu Ya Ngozi Kwa Watoto: Visababishi, Dalili Na Matibabu

Pumu ya ngozi ni ugonjwa wa ngozi unaofanya ngozi kuwasha, kuvimba na kuweka viupele vidogovidogo vyenye rangi nyekundu ...

5908
May 15, 2024
Read More
Unapokwenda kumuona daktari huwa unajielezaje?
Wellness

Unapokwenda kumuona daktari huwa unajielezaje?

Maongezi mazuri baina ya mgonjwa na daktari ni muhimu sana kuhakikisha tiba stahiki. Soma makala hii kuelewa njia nzuri ...

125
Aug 12, 2024
Read More
Mpox: Dalili, Kinga, na Hatua za Kuchukua
Viral diseases

Mpox: Dalili, Kinga, na Hatua za Kuchukua

Mpox ni ugonjwa wa virusi uliokuwa gumzo hivi karibuni nchini Tanzania. Je, unazijua dalili na njia za kujikinga? Soma z ...

644
Mar 12, 2025
Read More