Women Aug 28, 2024

Ijue siri kubwa ya kuzalisha maziwa ya kutosha

Medikea Doctor

Medikea Doctor

Medical Expert

143
Ijue siri kubwa ya kuzalisha maziwa ya kutosha

Uzalishaji wa maziwa unategemea kiwango cha homoni ya prolactin kinachopelekwa kwenye maziwa ya mama. Homoni ya prolactin inazalishwa kwa wingi kadri ziwa la mama linavyonyonywa mara nyingi au kukamuliwa mara nyingi. ⁣

⁣ Kwa hiyo siri kubwa kwa mama kupata maziwa ya kutosha ni kuhakikisha mtoto ana nyonya maziwa yake mara nyingi iwezekanavyo hasa siku za mwanzo baada ya mtoto kuzaliwa

Kama inawezekana hakikisha mtoto anaanza kunyonya ndani ya saa moja baada ya kuzaliwa. Katika wiki tatu za mwanzo mtoto anapaswa kunyonya angalau mara 12 kwa siku. ⁣

Kuwahi kumuanzishia mtoto maziwa ya kopo kutaathiri uwezo wako wa kuzalisha maziwa, kwa sababu mtoto atashiba na hivyo kushindwa kunyonya. Kama mwanao anashindwa kunyonya kutokana na ugonjwa au sababu nyingine hakikisha mwenyewe unakamua maziwa yako.⁣

Endapo umemnyonyesha mwanao mara nyingi zaidi na unahisi hupati bado maziwa ya kutosha na mwanao hashibi unaweza kujaribu kutumia baadhi ya vyakula vinavyoongeza maziwa au ongea na daktari wako akuandikie dawa ya kuongeza maziwa. ⁣

Lakini zingatia: Jambo moja muhimu ni kuhakikisha mtoto ananyonya, mvutishe ziwa mara nyingi kadri uwezavyo, angalau mara 12 kwa siku katika kipindi cha wiki tatu za mwanzo. ⁣Kama utafanya hivi na bado unadhani maziwa hayatoshi, tafadhali wasiliana na mtaalamu wetu wa lishe kupitia Medikea App.

Related Articles

Uti ni nini? Dalili zake na jinsi ya kujikinga
Women

Uti ni nini? Dalili zake na jinsi ya kujikinga

UTI inasababishwa na nini, dalili zake na jinsi ya kujinga

23724
Nov 6, 2024
Read More
Huu Ndio Utaratibu wa Kufanya Mazoezi Baada Ya Kujifungua Kwa Upasuaji
Women

Huu Ndio Utaratibu wa Kufanya Mazoezi Baada Ya Kujifungua Kwa Upasuaji

Huu Ndio Utaratibu Wa Kufanya Mazoezi Baada Ya Kujifungua Kwa Upasuaji

1624
Aug 12, 2024
Read More
“Tayari Nina Watoto Lakini Sipati Tena Mimba” - Ugumba wa aina ya pili
Women

“Tayari Nina Watoto Lakini Sipati Tena Mimba” - Ugumba wa aina ya pili

Fahamu sababu zinazosababisha ugumba kwa wenza ambao wameshapata Mtoto awali

240
May 15, 2024
Read More

More Health Insights

Nini cha kufahamu kuhusu ugonjwa wa ukoma
Women

Nini cha kufahamu kuhusu ugonjwa wa ukoma

Soma makala hii kujua zaidi kutusu ugonjwa wa ukoma, dalili na tiba yake.

839
Jan 27, 2024
Read More
Uti ni nini? Dalili zake na jinsi ya kujikinga
Women

Uti ni nini? Dalili zake na jinsi ya kujikinga

UTI inasababishwa na nini, dalili zake na jinsi ya kujinga

23724
Nov 6, 2024
Read More
Je ni sawa kuendelea kunyonyesha mtoto wakati una mimba nyingine?
Pregnancy

Je ni sawa kuendelea kunyonyesha mtoto wakati una mimba nyingine?

Makala hii inaelezea kwa kina zaidi⁣

2691
Aug 28, 2024
Read More