Women Sep 6, 2023

Saratani ya kizazi

Dr. Living Kimario

Dr. Living Kimario

Medical Expert

194
Saratani ya kizazi

NI NINI MAANA YA SARATANI YA KIZAZI?

Saratani ya kizazi ni aina ya saratani inayotokea kwenye utando wa ndani wa kizazi, uitwao endometriamu. Ni moja kati ya saratani zinazowakabili wanawake.

SABABU ZINAZOWEZA KUFANYA MWANAMKE KUWA KWENYE HATARI YA KUPATA SARATANI YA KIZAZI:

  • Uzito kupita kiasi,
  • Kukosa uwiano wa homoni (kama vile kuzidi kwa estrogeni),
  • Wanawake ambao hawajawahi kuwa na ujauzito,
  • Kuanza hedhi katika umri mdogo chini ya miaka 12,
  • Kikomo cha hedhi (menopausi) kutokea katika umri mkubwa zaidi ya miaka 55
  • Historia ya saratani ya kizazi kwenye familia

DALILI ZA SARATANI HII

  1. Kutokwa na Damu baada ya kikomo cha hedhi
  2. Maumivu Wakati wa Kujamiiana
  3. Kupoteza uzito bila sababu inayojulikana
  4. Kutokwa na Uchafu wa Muda Mrefu au Wa Kipekee: rangi ya kahawia au nyeusi, au uchafu wa kipekee ambao hauendani na mzunguko wa kawaida wa hedhi.

UCHUNGUZI WA SARATANI HII

  • Vipimo vya picha kama ultrasound,
  • Vipimo vya tishu kama vile biopsy(kuchukua kinyama),
  • Kusafisha kizazi (D&C) ili kukusanya sampuli za tishu kwa ajili ya uchunguzi.

MATIBABU

  1. Hutegemea hatua na aina ya saratani lakini zinaweza kujumuisha
  2. Upasuaji (kuondoa kizazi),
  3. Tiba ya mionzi,
  4. Chemotherapy,
  5. Tiba ya homoni,

Ni muhimu kuonana na wataalamu wa afya kwaajili ya uchunguzi na miongozo binafsi ikiwa wewe au mtu unayemjua anaweza kuwa katika hatari au amegunduliwa na saratani ya utando wa kizazi.

Related Articles

Uti ni nini? Dalili zake na jinsi ya kujikinga
Women

Uti ni nini? Dalili zake na jinsi ya kujikinga

UTI inasababishwa na nini, dalili zake na jinsi ya kujinga

40384
Nov 6, 2024
Read More
Ijue siri kubwa ya kuzalisha maziwa ya kutosha
Women

Ijue siri kubwa ya kuzalisha maziwa ya kutosha

Soma kujua jinsi ya kuzalisha maziwa ya kutosha kwa mama anaenyonyesha!

1396
Aug 28, 2024
Read More
Huu Ndio Utaratibu wa Kufanya Mazoezi Baada Ya Kujifungua Kwa Upasuaji
Women

Huu Ndio Utaratibu wa Kufanya Mazoezi Baada Ya Kujifungua Kwa Upasuaji

Huu Ndio Utaratibu Wa Kufanya Mazoezi Baada Ya Kujifungua Kwa Upasuaji

3597
Aug 12, 2024
Read More

More Health Insights

“Tayari Nina Watoto Lakini Sipati Tena Mimba” - Ugumba wa aina ya pili
Women

“Tayari Nina Watoto Lakini Sipati Tena Mimba” - Ugumba wa aina ya pili

Fahamu sababu zinazosababisha ugumba kwa wenza ambao wameshapata Mtoto awali

673
May 15, 2024
Read More
Genital Warts (Masundosundo): Tiba na jinsi ya kujikinga
Women

Genital Warts (Masundosundo): Tiba na jinsi ya kujikinga

Jifunze kuhusu Genital Warts, dalili, matibabu na kujikinga

11030
May 4, 2024
Read More
Ugonjwa wa Pumu: Vihatarishi, Dalili na Matibabu
Watoto

Ugonjwa wa Pumu: Vihatarishi, Dalili na Matibabu

Je wajua? Katika Tanzania, pumu ni tatizo kubwa la afya ya umma. Utafiti unaonyesha kuwa asilimia 10% hadi 20% ya watoto ...

1294
Feb 26, 2024
Read More