Women Jan 27, 2024

Nini cha kufahamu kuhusu ugonjwa wa ukoma

Dr Kuduishe Kisowile

Dr Kuduishe Kisowile

Medical Expert

875
Nini cha kufahamu kuhusu ugonjwa wa ukoma

Tanzania ni kati ya nchi zinazopewa kipaumbele katika mapambano dhidi ya ugonjwa huu ambao historia yake inaturudisha karne nyingi zilizopita.

Mwaka 2020, jumla ya visa 1,208 vya ukoma viligundulika nchini, ambapo mikoa ya Morogoro, Dar es Salaam na kisiwa cha Unguja iliongoza kwa visa hivi.

Ukoma ni ugonjwa unaosababishwa na vimelea vya bakteria waitwao Mycobacterium leprae, wanaoshambulia mishipa ya fahamu. Maambukizi ya Ukoma ni kwa njia ya hewa pekee kupitia majimaji kutoka mfumo wa upumuaji wa mtu mwenye maambukizi ya Ukoma akipiga chafya au kukohoa. Tofauti na dhana potofu iliyosambaa kwa jamii nyingi, ugonjwa wa Ukoma hauambukizwi kwa kugusana au kushikana mikono.

Dalili za Ukoma:

  • Vijinundu kwenye ngozi
  • Baka au mabaka mwilini yenye rangi ya shaba yasiyo na hisia
  • Mishipa ya fahamu kuvimba
  • Ganzi kwenye mikono na miguu

Njia pekee ya kujikinga dhidi ya madhara ya Ukoma ni kwa kufanya uchunguzi wa mara kwa mara na utambuzi wa mapema wa dalili zake ili kupata matibabu.

UKOMA UNATIBIKA! Iwapo mgonjwa wa ukoma atagundulika mapema, atapata matibabu ya dawa na kupona kabisa.

Tangu kuanzishwa kwa ugawaji wa dawa tiba za Ukoma kupitia Mpango wa Taifa wa Kifua Kikuu na Ukoma(NTLP) kwa kushirikiana na Shirika la Afya Duniani(WHO), visa vya ukoma nchini vimepungua kutoka visa 35,000 mnamo mwaka 1983 hadi kufikia takribani visa 1,200 mwaka 2020.

Madhara ya Ukoma:

  • Misuli kukosa nguvu
  • Kupooza
  • Matatizo ya macho na kupelekea upofu
  • Ulemavu wa mikono na miguu

Kutokana na madhara ya Ukoma, waathirika wengi wa ugonjwa huu hunyanyapaliwa na kutengwa na jamii kwa hofu ya kuambukiza wengine. Tunapoadimisha Siku ya Ukoma Duniani, nitoe wito kwa jamii kuepuka kuwanyanyapaa waathirika wa ugonjwa huu na kuendelea kuchukua tahadhari. Iwapo utaona dalili mojawapo, wahi katika kituo cha kutolea huduma za afya kilicho karibu nawe kwa matibabu zaidi.

Sources: NTLP, Wizara ya Afya, WHO Tanzania

Related Articles

Uti ni nini? Dalili zake na jinsi ya kujikinga
Women

Uti ni nini? Dalili zake na jinsi ya kujikinga

UTI inasababishwa na nini, dalili zake na jinsi ya kujinga

25634
Nov 6, 2024
Read More
Ijue siri kubwa ya kuzalisha maziwa ya kutosha
Women

Ijue siri kubwa ya kuzalisha maziwa ya kutosha

Soma kujua jinsi ya kuzalisha maziwa ya kutosha kwa mama anaenyonyesha!

249
Aug 28, 2024
Read More
Huu Ndio Utaratibu wa Kufanya Mazoezi Baada Ya Kujifungua Kwa Upasuaji
Women

Huu Ndio Utaratibu wa Kufanya Mazoezi Baada Ya Kujifungua Kwa Upasuaji

Huu Ndio Utaratibu Wa Kufanya Mazoezi Baada Ya Kujifungua Kwa Upasuaji

1865
Aug 12, 2024
Read More

More Health Insights

Upasuaji wa Kupunguza Uzito, Aina, Hatari na Urejeaji wa Afya
Health & Wellness

Upasuaji wa Kupunguza Uzito, Aina, Hatari na Urejeaji wa Afya

This blog post discusses bariatric surgery as a weight loss option for individuals with extreme obesity who have struggl ...

0
Mar 28, 2025
Read More
Strength Training Kwa Kupunguza Uzito Jinsi Inavyofanya Kazi
Afya na Siha

Strength Training Kwa Kupunguza Uzito Jinsi Inavyofanya Kazi

Blogi hii inaeleza jinsi mazoezi ya nguvu yanavyosaidia kupunguza uzito kwa kuongeza misuli, kuimarisha kimetaboliki, na ...

1
Mar 28, 2025
Read More
Je ni sawa kuendelea kunyonyesha mtoto wakati una mimba nyingine?
Pregnancy

Je ni sawa kuendelea kunyonyesha mtoto wakati una mimba nyingine?

Makala hii inaelezea kwa kina zaidi⁣

2980
Aug 28, 2024
Read More