Nutrition Aug 2, 2024

Vyakula vitano vinavyosaidia kupunguza kiungulia

Medikea Clinic

Medikea Clinic

Medical Expert

11077
Vyakula vitano vinavyosaidia kupunguza kiungulia

Kiungulia ni nini na kinasababishwa na nini? Kiungulia ni maumivu ya moto kwenye kifua, nyuma ya mfupa wa kifua. Maumivu haya hutokea baada ya kula, wakati wa kulala au wakati mtu ameinama.

Kiungulia hutokea wakati asidi ya tumbo inaporudi kwenye umio, mrija unaosafirisha chakula kutoka mdomoni hadi tumboni

KIUNGULIA KINAWEZA KUCHOCHEWA NA VITU KAMA VILE:

  • Vyakula vya mafuta au vya kukaanga.

  • Vinywaji vya kaboni, pombe, kahawa na vinywaji na vinywaji vya kafeini.

  • Bidhaa za machungwa.

  • Bidhaa za nyanya.

  • Chocolate

  • Milo mikubwa.

Ili kupunguza kiungulia inabidi kula vyakula vyenye asidi kidogo katika milo ya kila siku.

VYAKULA VITANO VINAVYOSAIDIA KUPUNGUZA KIUNGULIA

  • Vyakula vya alkali (Alkaline food): Vyakula hivi vina kiwango cha chini sana cha asidi hivyo husaidia kupunguza tatizo la kiungulia. Vyakula vya alkali huhusisha matunda kama vile ndizi na matikitiki, fenesi na karanga.

  • Tangawizi: Tangawizi ni mojawapo ya chakula cha asili kinachosaidia kupunguza tatizo la kiungulia. Tangawizi zina vitamin C na B, madini ya chuma, madini ya zink magnesium, calcium na phosphorus ambavyo pia hutumika kutibu tatizo la gesi tumboni na kiungulia.

  • Nyama zisizo na mafuta: Nyama kama vile kuku, bata mzinga na samaki hazina mafuta mengi hivyo zinaweza kutumika kupunguza hatari ya kiungulia kama zikichomwa au kuokwa. Hivyo ni vyema kuepuka kuzikaanga kwani vyakula vya kukaanga vina mafuta mengi na ni moja ya sababu kuu ya kiungulia.

  • Vyakula vya nafaka nzima: Vyakula vya nafaka nzima kama vile oatmeal, mkate na wali wa kahawia ni njia nzuri za kupambana na kiungulia kwani zinasaidia kunyonya asidi iliyojaa ndani ya tumbo, na nafaka hizi zimejaa vitamini na madini.

  • Maziwa mtindi: Maziwa ya mtindi ambayo hayana mafuta mengi husaidia kuzuia kiungulia na pia yana bakteria wazuri ambao huboresha usagaji wa chakula.

MUHIMU:

Ni vyema ukapata ushauri wa daktari kwanza kabla ya kuendelea na tiba yoyote ya mitishamba, kwa sababu vyakula vingine vinaweza kuwa na madhara kwako na mwingiliano wa madawa. Unaweza ku chat na daktari kupitia Medikea App.

Related Articles

No related articles found.

More Health Insights

Jinsi ya Kupunguza Kichefuchefu na Kutapika wakati wa Ujauzito
Pregnancy

Jinsi ya Kupunguza Kichefuchefu na Kutapika wakati wa Ujauzito

Jifunze njia za kupunguza Kichefuchefu na Kutapika wakati wa Ujauzito⁣

6734
Aug 28, 2024
Read More
Ijue siri kubwa ya kuzalisha maziwa ya kutosha
Women

Ijue siri kubwa ya kuzalisha maziwa ya kutosha

Soma kujua jinsi ya kuzalisha maziwa ya kutosha kwa mama anaenyonyesha!

1396
Aug 28, 2024
Read More
Dalili za Mimba Wiki ya Kwanza
Pregnancy

Dalili za Mimba Wiki ya Kwanza

Ujauzito ni mchakato wa kibaiologia ambao unahusisha mabadiliko makubwa katika mwili wa mwanamke. Katika wiki ya kwanza, ...

8024
Feb 25, 2025
Read More